Thursday, January 10, 2013

Chelsea yapingwa MBILI BILA na Swansea



 

 Michael Laudrup amakiri kuwa ushindi wa Swansea wa magoli mawili kwa bila dhidi ya Chelsea katika raundi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la ligi, ulikuwa wa kushangaza.
Makosa yaliyofanywa na mlinda lango wa Chelsea Branislav Ivanovic ilisababisha Michu na Danny Graham kuifungia Swansea magoli hayo katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa Stampford Birdge.
Raundi ya pili cha mechi hiyo itachezwa tarehe 23 mwezi huu katika uwanja wa nyumbani wa Swansea.
Chelsea ilithibiti mpira kwa asilimia kubwa lakini makosa hayo yaliyofanywa na Ivanovic yalisababisha matumaini ya Chelsea ya kufuzu kwa fainali za kombe hilo kudidimia.

No comments:

Post a Comment