Askari wawili wa Jeshi la Polisi wa Wilaya ya Ngara mkoani Kagera,
wameuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira na gari lao kuchomwa
moto, wakidhaniwa kuwa ni majambazi.
Tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Kasheshemisha, Kata ya Rugu Wilaya hiyo juzi saa 2:30 usiku.
Akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Karagwe
chini ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Darry Ibrahim Rwegasira na ya Mkoa
iliyoongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Phillipo Kalangi na
viongozi wengine wa serikali wilayani humo, Mwenyekiti wa Kijiji cha
Kasheshemisha, Sadick Mohammed, alisema walipata taarifa kutoka Kijiji
cha Rugu kuwa kuna majambazi walifika majira ya saa 12:00 jioni na
wakati wakijaribu kuondoka, wanakijiji waliweka kizuizi barabarani na
kuwaamuru wasimame.
Mihamed alisema watu hao hawakutii amri na kupita kwa nguvu katika eneo
hilo ndipo walipoamua kupiga simu kwa mwenyekiti huyo ambaye naye alitoa
taarifa kwa wananchi wake na kuziba barabara kwa mawe.
Alisema gari lao lilipofika Kijiji cha Kasheshemisha, lilikuta mawe
barabarani na kushindwa kupita ndipo wananchi waliwaamuru
wajisalimishe, lakini walikaidi na kuanza kufyatua risari hewani huku
wakitafuta njia ya kuwawezesha kutoroka.
Alisema walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili na kutokana na hasira
ya kurushiwa risasi, waliwapiga hadi kuwaua kisha walipopekua ndani ya
gari walikuta meno saba ya tembo.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, hasira za wananchi zilipanda zaidi
walipogundua mwenzao amejeruhiwa na risasi na kuamua kuyatoa meno hayo
ya tembo saba na kulitekeleza gari hilo lenye namba za usajili T.654
BNB.
Mohamed alisema mwanakijiji huyo, Jovinary Joseph aliyejeruhiwa na
risasi kwenye kiganja, alikimbizwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Karagwe
ya Nyakahanga kwa matibabu.
No comments:
Post a Comment