Monday, January 21, 2013

RC Lindi alazwa,Pinda amtembelea


Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila, amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo.

Akizungumza na NIPASHE jana mmoja wa wanafamilia ambaye alipokea simu ya Mkuu huyo wa mkoa alisema Mwananzila amelazwa hospitalini hapo tangu Jumatano ya wiki iliyopita.
Alisema Waziri Mkuu Mizengo Pinda amemtembela jana kumjulia hali na kwamba hata hivyo anaendelea vizuri na madaktari wamekuwa karibu naye kumtibu.

Naye Ofisa habari wa Muhimbili, Aminael Aligaesha, alisema Mkuu wa Mkoa wa Lindi hali yake inaendelea vizuri ukilinganisha na siku alipopelekwa hospitalini hapo.

No comments:

Post a Comment