Monday, January 7, 2013

CHADEMA YAMTIMUA MAKAMU MWENYEKITI WA BAVICHA

 Kamati ya Tendaji ya Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema (Bavicha), linadaiwa kumtimua uongozi na kisha kumvua uanachama Makamu Mwenyekiti wake Taifa, Juliana Shonza, pamoja na wanachama wengine wawili wa Baraza hilo
Mbali na Shonza, wanachama wengine wa Bavicha, ambao wamevuliwa uanachama na Kamati Tendaji ya Bavicha, wametajwa kuwa ni waliokuwa wagombea Uenyekiti wa Baraza hilo mwaka juzi, Habib Mchange na Mtela Mwampamba.

Mchange pia amewahi kuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema katika Jimbo la Kibaha Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, lakini akaangushwa na Mbunge wa sasa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sylivester Koka.(ipp media).

No comments:

Post a Comment